FAHAMU MATUMIZI MAPANA YA KITAMBULISHO CHA TAIFA
Ewe Mwananchi, sasa unaweza kutumia Namba yako ya Utambulisho wa Taifa (NIN)/Kitambulisho cha Taifa (NID) kupata huduma nyingi za kijamii, kiuchumi na kiusalama kama vile;
BOFYA NAMBA KUANGALIA KWANAMNA GANI UNAWEZA KUTUMIA KATIKA KAZI HUSIKA HAPO
CHINI.
- Kusajili Laini ya Simu (Sim Card Registration),
- Kusajili Namba Maalumu ya Mlipa Kodi (Tin),
- Kusajili Biashara/Kampuni – Brela,
- Kukata Hati ya Kusafiria ya Kielektroniki (E-Passport),
- Kukata Leseni ya Udereva,
- Kupata Huduma ya Afya,
- Kufungua Akaunti ya Benki,
- Kukopesheka Kirahisi kwenye Taasisi za Fedha,
- Kujiunga na Elimu Ngazi Mbalimbali,
- Kupata Mkopo wa Elimu ya Juu,
- Hati Miliki ya Kiwanja, Nyumba n.k,
- Kujidhamini na Kudhamini Wengine,
- Kitambulisho cha Taifa kutokana na kuwa na Kisilikoni (Cheap) kinaweza Kutumika kama Pochi ya Fedha ya Kielektroniki (E-Wallet) ambako unahifadhi fedha na kufanya malipo kwa kutumia Kitambulisho Chako,
- Kitambulisho kinaweza kutumika kama ATM CARD,
- Kwenye Maingio ya Malango Kielektroniki (E-Entrace),
- Daftari la Mahudhurio la Kielektroniki (Electronic Attendance),
- Mwananchi kuondokana na Adha ya Kubeba Utitiri wa Vitambulisho kwani sasa taarifa zote Muhimu za mwananchi zitapatikana katika Mfumo Mkuu wa Utambuzi wa Watu kwa Kutumia NIN/ Kitambulisho cha Taifa,
- Kinaweza kutumika kama hati ya Utambuzi wa Utaifa wa wananchi wanaovuka mipaka ndani ya nchi zilizoko katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwingineko.
- Vitaimarisha Utendaji Kazi Serikalini kwa Kuwa na Kumbukumbu Sahihi za Watumishi na Malipo ya Stahili zao, hasa wanapostahafu,
- Kupata Ruzuku za Pembejeo za Kilimo Kirahisi,
- Kujisajili kwenye Chama cha Ushirika (Kwa Wakulima, Wavuvi, Wafugaji Na Makundi Mengine),
- Kupata Msaada wa Tasaf Unaotolewa kwa Kaya Masikini,
- Kufungua Akaunti za Benki,
- Kuomba Ajira pamoja na Huduma Nyingine Nyingi.
TUMIA SASA NIN/NID YAKO KUPATA HUDUMA ZA KIJAMII, KIUCHUMI NA KIUSALAMA KIRAHISI
“NAMBA YAKO UTAMBULISHO WAKO”
0 Comments